Advertisement
Local News

NJIA MWAFAKA ZA KUACHANA NA MPENZI WAKO

Mdau wetu ameainisha njia zifuatazo kuwasaidia wadau kumaliza mahusiano na wenzi wao kwa amani

1. Kuwa na Uhakika na unachotaka kufanya: Kama huna uhakika juu ya hisia zako kwa mwenzi wako unapotaka kuvunja uhusiano bora usifanye hivyo maana utafanya moyo wako usiwe na maamuzi thabiti

2. Fikiria Sababu za Kuvunja Uhusiano: Unapojua sababu zinazopelekea wewe kuvunja mahusiano itakusaidia kutoa majibu ya uaminifu pale unapoulizwa

3. Maliza Mahusiano wewe Binafsi: Kama umekuwa na mpenzi wako kwa muda mrefu au kipindi chochote, uliwekeza muda na nguvu zako za kujenga mapenzi, hivyo ni busara mahusiano hayo ukayamaliza mwenyewe

4. Msikilize mwenzi wako: Hata kama umeshaamua na huwezi kubadili mawazo juu ya kuvunja mahusiano yenu, haina maana kuwa usimsikilize mwenzi wako

5. Kuwa Mtulivu na Makini: Unahitaji kuumaliza uhusiano na kuondoka mahali mlipo. Hata hivyo, ni busara kuwa mtaratibu na mpole

Je, nini uzoefu wako kuhusu kuacha au kuachwa katika mahusiano?

Tambua Africa Reporter

Blogger and news writer at Tambua Africa News.

Related Articles

Hi! Post Your Comment Here.

Back to top button

Adblock Detected

Kindly Allow Ads to view this page.